About

www.facebook.com/archileusanatory/pambazuabongo

Wajumbe wa Bunge la Katiba wameelezwa kuwa yeyote atakayesema uongo wakati wa kujadili kwa lengo la kuboresha Rasimu ya Pili ya Katiba, ataadhibiwa kwa kuzuiliwa kuhudhuria vikao vitatu.
Hayo yalielezwa na Mtaalamu wa Sheria ambaye pia ni mmoja wa Wajumbe wa Kamati iliyoboresha Rasimu ya Kanuni zinazoongoza Bunge hilo, Dk. Tulia Ackson, wakati akitoa ufafanuzi wa kanuni kwa wabunge bungeni.
“Makatazo yanayopatikana katika kanuni ya 46.-(1) ni kusema uongo, kutumia majina ya waasisi na marais kwa dhihaka, kuzomea na kupiga kelele na mengine kama yanavyoonekana kwenye ibara hiyo, hivyo ni vizuri kuhakikisha tunazingatia kanuni ili twende sawa wakati wa mijadala,”  alisema.
Pamoja na kuelezea vipengele vingine vilivyo katika ibara hiyo, Dk. Ackson alisema mjumbe anapewa kinga na kanuni hizo juu ya alichosema ndani ya mijadala bungeni, ikiwa amefanya rejea katika kumbukumbu rasmi. 
“Ikiwa mjumbe anazungumza, mjumbe mwingine akafuata taratibu za kutoa taarifa. Atakaporuhusiwa na mwenyekiti wa Bunge na ikaelezwa kuwa kinachoelezwa na mzungumzaji ni uongo, mzungumzaji atapata muda wa kujibu madai yaliyotolewa dhidi ya mazungumzo yake,’ alisema.
Kwa mujibu wa Dk. Ackson, kanuni zinaeleza kuwa mzungumzaji atatakiwa kuthibitisha alichoeleza kuwa ni sahihi na kwamba akishindwa kufanya hivyo, itachukuliwa kuwa amesema uongo na atastahili adhabu husika.

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top