STAA wa filamu Bongo,
Kulwa Kikumba ‘Dude’ amewatoa nishai viongozi wa Bongo Muvi kwa kueleza
kuwa, risala iliyosomwa siku ya ‘bethidei’ yao ya kutimiza miaka mitatu
imepotosha ukweli.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Dude alisema ameshangaa kusikia
kwenye risala hiyo kuwa waanzilishi wa umoja huo ni Kanumba, Sajuki,
Jimmy Mafufu na wengineo wakati ukweli hauko hivyo.
“Ile risala imepotosha, Bongo Muvi ilianzishwa na wasanii wa muziki
na filamu wakiwemo mimi, William Mtitu, H.Baba, Simon Mwakifwamba,
MwanaFA na Fid Q na wengineo kwa lengo maalum, nimeshangaa kusikia
vile,” alisema Dude huku akisisitiza kuwa, yeye hajisifii ila ukweli
usipindishwe.
Home
»
»Unlabelled
» KALI; DUDE AWATOA NISHAI BONGO MUVI, CHEKI MWENYEWE HAPA
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
0 maoni:
Chapisha Maoni