About

www.facebook.com/archileusanatory/pambazuabongo


Taarifa kutoka Kenya naambiwa watu wanne waliokua kwenye ndege iliyokua ikipaa kutoka uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta Nairobi kuelekea Mogadishu Somalia wamefariki dunia baada ya Ndege hiyo kuanguka katika eneo la Utawala dakika chache baada ya kupaa,
Ajali hiyo imetokea alfajiri ya July 02 na inaaminika kwamba ndege hiyo ilikua iondoke mapema kusafirisha zao la Mirungi na bidhaa zinginezo kuelekea Somalia.
Walinzi wawili walijeruhiwa mmoja ametibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani huku mmoja amelazwa katika hospitali ya mama Lucy,kwa mujibu wa mkuu wa polisi Jijini Nairobi Benson kibue amethibitisha ajali hiyo na kusema kuwa Ndege hiyo yenye nambari 5Y-CET ilianguka kwenye paa la jengo la kibiashara likijaribu kutua ghafla na kushika moto papo hapo likiteketeza watu wanne waliokua ndani.
Polisi wanaendelea na uchunguzi kwenye mabaki ya ndege hiyo kuona iwapo kuna waasilika zaidi.


>>>>>>>BBC<<<<<<<<

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top