Gari lililotekwa ambalo ni sehemu ya usalama wa Rais wa Kenya limeonekana nchini Uganda.
Gari hilo aina ya BMW lilichukuliwa katika siku ya Jumatano katika mji mkuu wa Nairobi.
Kiongozi wa Interpol nchini Uganda, Assan Kasingye, aliiambia BBC kwamba gari hilo litaendeshwa kurudishwa Nairobi.
Taarifa za sasa za polisi wa Kenya ni kwamba kuna angalau utekaji wa magari matatu katika mji mkuu kila siku.
Mwandishi wa BBC wa Nairobi Paul Nabiswa anasema wizi huo ulipata
kutangazwa kwa kiasi kikubwa na vyombo vya habari, pamoja na kwamba
msemaji wa Rais Uhuru Kenyatta kujaribu kukwepa jukumu hilo.
Msemaji huyo alikwishasema ilikuwa sio sehemu ya magari ya usalama wakati na kwamba lilikuwa gari la polisi.
Lakini magazeti ya Kenya yalithibitisha kuwa gari hilo liliendeshwa na
mkaguzi wa polisi ambaye ni sehemu ya wafanyakazi wa usalama wa rais,
alisema ripota wao.
Waliongeza kwamba watu wapatao watatu wameshakamatwa tayari kwa
kuhusishwa na wizi huo mjini Nairobi, Nakuru, mji wa
kaskazini-magharibi, na Bungoma, mji ulipo mpaka na Uganda.
0 maoni:
Chapisha Maoni