About

www.facebook.com/archileusanatory/pambazuabongo

Magari ambayo ni sehemu ya ulinzi wa Rais Kenyatta yanapaswa kulindwa sana.
Magari ambayo ni sehemu ya ulinzi wa Rais Kenyatta yanapaswa kulindwa sana.
Gari lililotekwa ambalo ni sehemu ya usalama wa Rais wa Kenya limeonekana nchini Uganda.
Gari hilo aina ya BMW lilichukuliwa katika siku ya Jumatano katika mji mkuu wa Nairobi.
Kiongozi wa Interpol nchini Uganda, Assan Kasingye, aliiambia BBC kwamba gari hilo litaendeshwa kurudishwa Nairobi.
Taarifa za sasa za polisi wa Kenya ni kwamba kuna angalau utekaji wa magari matatu katika mji mkuu kila siku.
Mwandishi wa BBC wa Nairobi Paul Nabiswa anasema wizi huo ulipata kutangazwa kwa kiasi kikubwa na vyombo vya habari, pamoja na kwamba msemaji wa Rais Uhuru Kenyatta kujaribu kukwepa jukumu hilo.
Msemaji huyo alikwishasema ilikuwa sio sehemu ya magari ya usalama wakati na kwamba lilikuwa gari la polisi.
Lakini magazeti ya Kenya yalithibitisha kuwa gari hilo liliendeshwa na mkaguzi wa polisi ambaye ni sehemu ya wafanyakazi wa usalama wa rais, alisema ripota wao.
Waliongeza kwamba watu wapatao watatu wameshakamatwa tayari kwa kuhusishwa na wizi huo mjini Nairobi, Nakuru, mji wa kaskazini-magharibi, na Bungoma, mji ulipo mpaka na Uganda.

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Top