Kuchaguliwa kwa Waziri wa Ujenzi nchini Tanzania Daktari John Magufuli
kubeba bendera ya chama tawala cha CCM katika uchaguzi mkuu wa mwezi
Oktoba mwaka huu kumepokelewa na hisia tofauti na wananchi nchini humo.
Ametumikia awamu tatu za uongozi akiwa waziri. Daktari Magufuli
alichaguliwa mwishoni mwa wiki na mkutano mkuu wa CCM mjini Dodoma baada
ya kuwashinda washindani wake Balozi Amina Salum Ali na Daktari Asha
Rose Migiro. Kwa mara ya kwanza katika historia ya Chama cha Mapinduzi,
Daktari Magufuli atakuwa na mgombea mwenza mwanamke Samia Suluhu. Sammy
Awami anaripoti zaidi kutoka Dodoma.
Home
»
»Unlabelled
» Uchaguzi wa Magufuli wazua hisia tofauti TZ
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
0 maoni:
Chapisha Maoni